Thursday, February 8, 2018

Kufanyika kwa Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji

Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha, na Uwekezaji unaendelea kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Masharik Jijini Arusha. Mkutano huu unafanyika kwa muda wa siku tatu  tarehe 7 hadi 9 Februari, 2018.

Pamoja na mambo mengine Mkutano huu unatarajiwa kufanya mambo yafuatayo:
·         Kujadili kuhusu vikwazo vya biashara vya muda mrefu visivyo vya kiushuru

·         Kupokea taarifa ya mwenendo wa sasa wa soko kati ya Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EU-EAC);

·         Kupokea taarifa ya Biashara na Uwekezaji ya mwaka 2016 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Taarifa hii inaainisha mafanikio, changamoto na kutoa mwenendo wa biashara na uwekezaji ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki; na

·         Kupokea na kuridhia mwongozo wa Vituo vya Utoaji Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) ambao utatoa utaratibu wa namna ya kuviendesha vituo hivyo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mkutano huu unafanyika ili kujadili na kutoa ufumbuzi wa masuala mbalimbali kama ilivyoagizwa kwenye Mikutano iliyopita ya Wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mkutano huu unafanyika katika ngazi tatu; ngazi ya Wataalamu, ngazi ya Makatibu Wakuu na hatimaye katika ngazi ya Mawaziri.

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
 8 Februari 2018





Kaimu Mkurugezi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule akizungumza kwenye Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezajia la Jumuiya ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki


Wajumbe kutoka Tanzania wakifuatilia Mkutano 

Naibu Katibu Mkuu, Biashara na Uwekezaji Tanzania bara  Prof. Joseph Buchweishaija (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Bw. Ally K. Juma (kulia), wakifuatilia Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji katika ngazi ya Matibu Wakuu

Sehemu ya Wajumbe kutoka nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki Wakifuatilia Mkutano

Naibu Katibu Mkuu wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar Bw. Ally K. Juma akifafanua jambo kwenye Mkutano wa Dharura wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji ngazi ya Makatibu Wakuu

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.