Friday, February 23, 2018

Naibu Waziri Kolimba aongoza maadhimisho ya siku ya Taifa la Kuwait

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba (Mb.) akizungumza katika hafla ya kuadhimisha siku ya Taifa la Kuwait. Katika hafla hiyo Dkt.Kolimba ambaye alikuwa mgeni rasmi alitumia fursa hiyo kulipongeza taifa hilo na kuahidi kuendeleza ushirikiano  uliopo kati ya Tanzania na Kuwait.Pia alimpongeza Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem kwa juhudi zake za kuboresha na kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait hususan kwa kuchangia  sekta mbalimbali zikiwemo huduma za kijamii kama elimu na afya. Hafla  hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Mabalozi walio hudhuria hafla hiyo wakimsikiliza kwa makini Dkt. Kolimba (hayupo pichani).
Dkt. Kolimba akiendelea kuzungumza huku wageni waalikwa wakimsikiliza.

Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem naye akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Sehemu nyingine ya Mabalozi wakimsikiliza kwa makini Mhe. Najem akihutubia.
Dkt. Kolimba akishiriki katika zoezi la kukata keki kwenye hafla hiyo.
Dkt. Kolimba akipokea picha iliyochorwa kwa Mkono kutoka kwa Balozi Najem.
Dkt. Kolimba akisalimiana na Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim walipokutana kwenye hafla hiyo.
Dkt. Kolimba akisalimiana na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mhe. Monica Patricip Clemente Mussa. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba.










No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.