Friday, February 23, 2018

Naibu Waziri akutana na Mjumbe Maalum kutoka Poland

Naibu Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akiwa katika mazungumzo na Mjumbe maalum kutoka Nchi ya Poland Mhe. Krzysztof Szczerki alipomtembelea Wizarani, tarehe 22 Februari, Dar es salaam. Mazungumzo yao yalilenga zaidi jinsi ya kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Nchi ya Poland katika maeneo mbalimbali ya maendeleo.

  Mhe. Dkt Kolimba na Mhe. Szczerki wakiendelea na mazungumzo, wanaofuatilia   wa kwanza kushoto ni Balozi wa Poland nchini Mhe. Krzysztof Buzalski pamoja na wajumbe waliombatana nao kutoka Ubalozini na wa kwanza  kulia ni Bw. Salvatory Mbilinyi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika  na Maafisa kutoka Wizarani.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.