Thursday, February 1, 2018

Waziri Mahiga Afungua Kongamano la Kwanza la Biashara Jamhuri ya MheKorea

Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia mamia ya wafanyabiashara waliofurika kwenye Ukumbi wa Hana kuhudhuria Kongamano la Kwanza la Biashara lililofanyika Mjini Seoul Jamhuri ya Korea tarehe 31 Januari, 2018.
Mheshimiwa Matilda Masuka Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Jamhuri ya Korea akitoa neno la ukaribisho wakati wa Kongamano la Kwanza ambalo liliandaliwa na Ubalozi wa Tanzania. 


Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania, akitoa taarifa kuhusu mazingira ya uwekezaji Tanzania na fursa zinazoweza kupatikana kwa wawekezaji wa Korea Kusini iwapo wataamua kuja kuwekeza Tanzania.

Makamu Mwenyekiti wa Korea Chamber of Commerce and Industries akishuka kutoka kwenye eneo la kuhutubia ambapo alitoa mwelekeo wa biashara baina ya Korea Kusini na Afrika na hatimaye fursa za kufunguka biashara na uwekezaji baina ya Korea Kusini na Tanzania. Alisihi wanachama wa taasisi hiyo kongwe ya biashara nchini humo, kuangalia Tanzania kama mshirika imara kiuchumi barani Afrika.


Bw. Masuka, ambaye ni mume wa Mheshimiwa Balozi Matilda Masuka akiendesha kongamano hilo ambapo mwanafunzi Mtanzania anayesoma Seoul, akitafsiri kwa lugha ya Kikorea.

Mheshimiwa Waziri Mahiga akiwa kwenye meza kuu kabla ya Kongamano kuanza.



Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania akitoa mada wakati wa Kongamano hilo lililofanyika Jijini Seoul Korea Kusini tarehe 31 Januari 2018.

Kanali (Mstaafu) Joseph Simbakalia, Mkurugenzi Mkuu wa EPZA Eneo Maalum la Uwekezaji, akitoa mada wakati wa Kongamano la Kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea. Kongamano hilo lilifanyika sambamba na ufunguaji rasmi wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo tarehe 31 Januari, 2018. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.