Monday, February 26, 2018

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mwakilishi wa Taasisi ya Aga Khan

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa masuala ya Diplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani.Katika mazungumzo yao walijadili kuhusu ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Taasisi hiyo katika sekta ya Elimu na Afya. Mazungumzo hayo ambayo yalihudhuriwa na Bw. Amin Kurji alieambatana na Balozi Lalani yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Jijini Dar es Salaam.   
Balozi Lalani akimweleza jambo Prof. Mkenda.
Mazungumzo yakiendelea.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Mkenda akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Lalani (wa tatu kushoto), Bw. Kurji (wa tatu kulia), Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Sheria, Bibi Caroline Chipeta (wa pili kulia), Katibu wa Katibu Mkuu, Bi. Bertha Makilagi (wa kwanza kushoto) na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Elisha Suku.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.