Monday, February 12, 2018

Hafla ya chakula cha jioni kwa Wajumbe wa Baraza la Wakimbizi Duniani yafana

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akizungumza kwenye hafla ya chakula cha jioni na Wajumbe wa Baraza la Wakimbizi Duniani. Hafla hiyo iliandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuhudhuriwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya nne na Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Wakimbizi Duniani, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mwenyekiti wa Baraza hilo la Wakimbizi Duniani Mhe. Lloyd Axworthy, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani,  Balozi Simba Yahaya (hawapo pichani).  Hafla hiyo imefanyika katika Hotel ya Hyatt Regancy, Jijini Dar es Salaam. 
Sehemu ya wageni waliohudhuria hafla hiyo.
Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Gerald Mbwafu (wa kwanza kushoto), Afisa Mambo ya Nje, Bi.Ramla Hamis (wa pili kutoka  kushoto) pamoja na Mjumbe wa Baraza la  Wakimbizi Duniani nao wakiwa katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Baraza hilo la Wakimbizi Duniani, Mhe. Lloyd Axworthy naye akitoa neno la shukrani kwa Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mapokezi yao hapa nchini.
Mhe. Axworthy akiendelea kuzungumza huku meza kuu wakimsikiliza kwa makini
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza hilo nao wakiendelea kumsikiliza Mhe. Axworthy (hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa wakiendelea kumsikiliza Mhe. Axworthy alipokuwa akizungumza.  
Bi. Nguse Nyerere, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa akisherehesha kwenye hafla hiyo
Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (wa kwanza kulia), pamoja na Mhe. Lloyd Axworthy wakifurahia jambo kwa pamoja.










No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.