Friday, February 16, 2018

Mhe. Rais Magufuli awaapisha Mabalozi wa Tanzania nchini Nigeria na Sweden


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimwapisha Bw. Muhidin Ally Mboweto kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria. Hafla ya uapisho imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Februari, 2018


Balozi Mboweto akisaini mara baada ya kula kiapo cha kuiwakilisha Tanzania nchini Nigeria
Mhe. Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Balozi Mboweto
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Dkt.John Pombe Joseph Magufuli akimwapisha Dkt. Wilbroad Peter Slaa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden.
Balozi Slaa akisaini kiapo chake
Mhe. Rais Magufuli alimkabidhi Balozi Slaa vitendea kazi
Balozi Mboweto na Balozi Slaa kwa pamoja wakila kiapo cha Maadili ya Viongozi mbele ya Mhe. Rais Magufuli
Mhe. Rais Magufuli kwa pamoja na Balozi Mboweto na Balozi Slaa (walioketi) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba alipokuwa akitoa nasaha zake kwa Mabalozi hao mara baada ya kuapishwa.
 Wakuu wa Vyombo vya Usalama nchini na wageni wengine waalikwa wakimsikiliza Dkt.Kolimba (hayupo pichani)
Sehemu ya viongozi mbalimbali na wageni waalikwa  wakiwa kwenye hafla ya kuapishwa kwa Balozi Mboweto na Balozi Slaa (hawapo pichani). Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi


Mhe. Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mboweto mara baada ya kumwapisha
Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Slaa mara baada ya kumwapisha

 Mhe. Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi walioapishwa na viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi (wa pili kulia) na  Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (kushoto)
 Mhe. Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi walioapishwa na viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (wa pili kushoto), Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (wa pili kulia), Naibu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi (kushoto) na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Wizara ya Mambo aya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.