Friday, February 9, 2018

Katibu Mkuu Mambo ya Nje akutana na Mwakilishi wa Aga Khan

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akizungumza na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Aga Khan, Bw. Amin Kurji alipomtembelea katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 09 Februari 2018.
Mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Bw. Kurji yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano na shughuli za maendeleo ambazo zimekuwa zikifanywa na Shirika la Aga Khan nchini katika kuhudumia wananchi hususan katika sekta ya Afya na Elimu. 


Mazungumzo yakiendelea, kulia ni wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.