Saturday, February 10, 2018

Waziri Mahiga awa mgeni rasmi maadhimisho ya miaka 39 ya Taifa la Iran

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akihutubia wakati wa maadhimisho ya 39 ya  Taifa la Iran. Mhe. Mahiga ambaye alikuwa alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alitumia fursa hiyo kuelezea mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Tanzania na Iran katika sekta mbalimbali zikiwemo biashara na elimu. Aidha alilipongeza taifa hilo kwa hatua kubwa ya maendeleo wanayopiga hususan katika matumizi ya teknolojia.
Waziri Mahiga akiendelea kuzungumza kwenye maadhimisho hayo.
Sehemu ya Mabalozi wanao ziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia hotuba ya Waziri Mahiga (hayupo pichani).
Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe.Mousa Farhang naye akitoa hotuba wakati wa maadhimisho hayo ya 39 ya taifa lao
Sehemu ya viongozi wa dini pamoja na wageni waalikwa nao kwa pamoja wakisikiliza hotuba kwenye maadhimisho hayo.
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nao wakiwa katika hafla hiyo. 
Sehemu ya raia wa Iran wanaoishi nchini na wageni waalikwa wakifatilia matukio wakati wa maadhimisho hayo
Waziri Mahiga akizungumza jambo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe.Mousa Farhang
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga (kulia) pamoja na Katibu wa Waziri Bw. Gerald Mbwafu nao walihudhuria hafla hiyo
Waziri Mahiga akisalimiana na Sheikh al Hadi Musa Salim, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam walipokutana kwenye hafla hiyo.  
Waziri Mahiga akisalimiana na Balozi wa Algeria nchini Tanzania Mhe.Saad Belabed walipokutana nae kwenye hafla hiyo.
Picha ya pamoja.













No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.