Wednesday, February 28, 2018

Mhe. Balozi Simba afunga mafunzo kwa Maafisa wa polisi



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, ambaye pia alikuwa mgeni rasmi, Mhe. Balozi Hassan Y. Simba akisoma hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu ya Maafisa wa Polisi, Mafunzo hayo yemetolewa na chuo cha mambo ya usalama cha Naif Arab University for Security Science, hafla hiyo imefanyika tarehe 28 Februari,2018, katika Hotel ya Hyatt Regency, Dar es Salaam.
 Balozi wa Tanzania nchini Saud Arabia, Mhe. Balozi Hemed Mgaza akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje katika hafla hiyo.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Balozi Hassan Y. Simba (katikati), Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia , Mhe. Balozi Hemed Mgaza (kulia), anayefuata ni Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Jeshi la Polisi, Commandor Nsato Marijani. wa pili kutoka mwisho kushoto ni Balozi wa Saudi Arabia nchini Mhe. Balozi Mohamed Ben Mansour Al Malek wakifuatilia shughuli hiyo.
Sehemu ya wageni wakifuatilia ufunguzi huo.
    
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo Bw. Hangi Mgaka akipokea cheti katika hafla hiyo
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Ramadhani M. Mwinyi akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mhe. Mohamed Ben Mansour Al Malek 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Balozi Hassan Y. Simba akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mhe. Mohamed Ben Mansour Al Malek 



Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.