Friday, November 30, 2012

Hafla ya Kufungua Jengo Jipya la Makao Makuu ya EAC

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Serikali na wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika hafla ya ufunguzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha tarehe 28 Novemba, 2012

Mhe. Mwai Kibaki, Rais wa Kenya na Mwenyekiti wa EAC akiwasilisha hotuba yake wakati wa hafla ya ufunguzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mhe. Rais Kibaki akitoa cheti kwa mmoja wa Wahandisi waliofanikisha ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mwakilishi wa Serikali ya Ujerumani naye akitoa hotuba fupi katika hafla hiyo. Serikali ya Ujerumani ndiyo iliyodhamini ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya EAC

Mhe. Rais Kikwete wa kwanza kushoto akiwa na baadhi ya viongozi wenziwe wa EAC wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya EAC.

Mhe. Rais Kikwete (katikati) na Viongozi wenziwe wa EAC wakiwa katika moja ya vyumba vya jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Mhe. Rais Kikwete wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa EAC mjini Arusha.

Mwakilishi wa Serikali ya Ujerumani na wa EAC wakiweka saini Mkataba wa kushirikiana kiuchumi kati ya Ujerumani na EAC

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akibadilishana mawazo na Bw. Richard Sezibera, Katibu Mkuu wa EAC wakati wa hafla ya kufungua Jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Wanafunzi wa Shule ya Msingi wakitoa burdani wakati wa hafla ya kufungua jengo la Makao Makuu ya EAC mjini Arusha

Wednesday, November 28, 2012

Rais Kikwete ahutubia Mkutano wa Tatu wa Bunge la Afrika Mashariki

m

Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Margaret B. Ziwa akimkaribisha Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipowasili kwenye Makao Makuu ya Jumuiya hiyo kwa ajili ya kuwahutubia Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki mjini Arusha tarehe 27 Novemba, 2012.

Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Margaret Ziwa akitoa salamu za kumkaribisha Mhe. Rais Kikwete kuhutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki. Anayeoneka pembeni mwa Mhe. Ziwa ni Mhe. Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe.  Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisisitiza jambo wakati alipokuwa anawahutubia Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki mijini Arusha tarehe 27 Novemba,2012
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na wageni waalikwa wakimsikiliza Mhe. Rais Kikwete alipowahutubia.

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na  Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Ziwa mbele ya Jengo Jipya la Makao Makuu ya EAC.

Bw. David Mwakanjuk (katikati), Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha (kushoto) Mhe. Magesa Mulongo kabla ya kikao cha Bunge la EAC kuanza tarehe 27 Novemba, 2012. Mwingine katika picha ni Afisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.

Tuesday, November 27, 2012

Jengo Jipya la Makao Makuu ya EAC kufunguliwa rasmi

Muonekano wa mbele wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambalo litafunguliwa rasmi na Wakuu wa Nchi wa EAC siku ya Jumatano tarehe 28 Novemba, 2012 Jijini Arusha. Wanaoonekana kwa mbali ni Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakijiandaa na shughuli za ufunguzi huo.

Friday, November 23, 2012

Mkurugenzi wa Idara ya Asia akutana kwa mazungumzo na Balozi wa India nchini

Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na India na Mhe. Debnath Shaw, Balozi wa India hapa nchini.

Balozi Shaw akielezea jambo huku Balozi Mbelwa akimsikiliza.
Balozi Mbelwa (wa pili kutoka kulia) akifafanua jambo kwa Balozi Shaw (wa pili kutoka kushoto) wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bw. Kunal Roy (kushoto), Afisa kutoka Ubalozi wa India hapa nchini na Bi. Redemptor Tibaigana (kulia), Afisa kutoka Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Kimataifa.
Balozi Mbelwa akiagana na Balozi Shaw mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Mkurugenzi wa Idara ya Asia azungumza na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Sumitomo ya Japan

Balozi Mbelwa Kairuki (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Wizarani Bw. Hitokazu Okado, Makamu wa Rais wa  Kampuni ya Sumitomo ya Japan alipofika kwa mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya uwekezaji.
Balozi Mbelwa akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Bw. Okado.
Bw. Okado akimuelezea Balozi Kairuki shughuli mbalimbali zinazofanywa na Kampuni ya Sumitomo.
Balozi Kairuki (wa tatu kutoka kulia) akimsikiliza Bw.Okado  (wa pili kutoka kushoto) wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bw. Tetsujiro Tani ( kushoto) Mkurugenzi Msaidizi wa Kampuni  ya Sumitomo, Bi. Redemptor Tibaigana (Kulia), Afisa kutoka Idara ya Asia na Australasia, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Bw. Hasnein GulamHussein, Mkurugenzi wa Kampuni ya Sumitomo hapa nchini.

Mkurugenzi wa Asia akutana na Mwakilishi wa Kampuni ya NEC Afrika kutoka Japan

Balozi Mbelwa Kairuki (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akimkaribisha Wizarani Bw. Koji Nakamura, Mkurugenzi wa Kampuni ya NEC Afrika ya Japan inayojishughulisha na masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Bw. Nakamura alifika Wizarani kwa lengo la kuitambulisha teknolojia mpya  inayotumiwa na Kampuni yake ikiwa ni jitihada za kuimarisha sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano hapa nchini.

Balozi Kairuki akiwa katika mazungumzo na Bw. Nakamura kuhusu masuala ya Teknolojia hapa nchini.

Balozi Kairuki akimsikiliza Bw. Nakamura alipokuwa akimuelezea masuala mbalimbali kuhusu teknolojia hiyo.

Bw. Nakamura akimuonyesha Balozi Kairuki moja ya teknolojia wanayoitumia katika masuala mbalimbali ya mawasiliano.

Bw. Ryoji Metsuoka (kushoto), mmoja wa Wataalam aliyefuatana na Bw. Nakamura (katikati) akifafanua jambo kwa Balozi Kairuki kuhusu Teknolojia hiyo ya kisasa ya mawasiliano. 

Thursday, November 22, 2012

Minister Membe bids farewell to Uganda High Commissioner


Ambassador Ibrahim Mukiibi, High Commissioner of the Republic of Uganda signing a visitors' book today at Hon. Bernard K. Membe's office. (photo by Tagie Daisy Mwakawago)


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation shares a good laugh with Ambassador Ibrahim Mukiibi, High Commissioner of the Republic of Uganda in the United Republic of Tanzania.  Ambassador Mukiibi, who has ended his tour of service, paid a courtesy visit to say goodbye to the Minister in his office today in Dar es Salaam.  (photo by Tagie Daisy Mwakawago)


Hon. Membe and Ambassador Mukiibi during their discussion.  Others are Foreign Service Officers in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.  (photo by Ally Kondo Seif)

  



TANZANIA YALAANI MASHAMBULIZI YA M23



Mhe. Bernard K. Membe (Mb) (katikati) akilaani mashambulizi ya kikundi cha waasi cha M23 kilichoteka mji wa Goma, Mashariki mwa Congo DRC.   Waziri Membe aliyasema hayo alipokuwa katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano, Wizara ya Mambo ya Nje, mjini Dar es Salaam.  Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. John M. Haule na Kushoto ni Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Wizarani. 


Mhe. Waziri Membe akiongea na Waandishi wa Habari.


Waziri Membe akieleza historia ya kikundi cha waasi cha M23 kilivyojiita jina hilo tarehe 23 Machi, 2009.  Kushoto ni Balozi Yahya.

Mhe. Bernard K. Membe (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akitoa msimamo wa Tanzania kuhusu vitendo vya kikundi cha waasi  cha M23 kilichopo Mashariki mwa Congo DRC.  Kushoto ni Balozi Simba Yahya.


Picha zote na Tagie Daisy Mwakawago



TANZANIA YALAANI MASHAMBULIZI YA M23

Na ALLY KONDO SEIF


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) amelaani kitendo cha kikundi cha M23 kuteka mji wa Goma na kutishia kuteka miji mingine ya Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Mhe. Waziri alitoa msimamo huo wakati alipozungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam tarehe 22 Novemba, 2012.

Mhe. Waziri alisema kuwa hali ya usalama mjini Goma ni mbaya kutokana na mashambulizi hayo ya M23 na hali hiyo ikiachwa iendelee, Tanzania itaathirika kwa kiasi kikubwa kwani watu wengi watakimbilia hapa nchini kama wakimbizi.

Aidha, Mhe. Waziri alisikitishwa na kikundi cha M23 cha kupuuza wito uliotolewa na viongozi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Sekretarieti ya Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) wa kusitisha mapigano hayo.

Mhe. Waziri aliendelea kueleza kuwa Tanzania inasikitishwa na jeshi la Umoja wa Mataifa la MONUSCO lililopewa jukumu la kulinda amani Mashariki ya DRC kwa kushindwa kuchukuwa hatua za kukomesha mashambulizi hayo na badala yake kuwa mashuhuda wa mashambulizi yanayofanywa na kikundi cha M23 dhidi ya Serikali na wananchi wa kawaida.

Aliuomba Umoja wa Mataifa utoe mamlaka ili MONUSCO iwe na uwezo wa kisheria wa kukabiliana na waasi wa M23 kama sura ya 7 ya Umoja wa Mataifa inavyoelekeza badala ya kutumia sura ya 6 ya Umoja wa Mataifa inayosisitiza umuhimu wa kulinda amani bila kujibu mashambulizi.

Kuhusu jitihada zinazofanywa na SADC kwa kushirikiana na ICGLR za kutafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro huo, Mhe. Membe alisema kuwa mwezi Agosti, 2012 Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hizo walikutana mjini Kampala, Uganda na kuamua kuunda kikosi cha kulinda amani ili kitumwe Mashariki ya DRC. Tanzania iliahidi kuchangia batalioni moja lakini kikosi hicho cha kulinda amani hakijapata ridhaa ya Umoja wa Mataifa.

Umoja wa Mataifa hautaki kutoa ridhaa ili kikosi hicho kipelekwe DRC kwa hoja kuwa tayari jeshi la Umoja wa Mataifa lipo nchini DRC.

Mhe. Waziri alihitimisha Mkutano wake kwa kutoa taarifa kuwa nchi za SADC na ICGLR zitakuwa na mkutano nchini Uganda kuanzia siku ya Ijumaa tarehe 23 Novemba, 2012 kujadili hatua za haraka za kuchukuwa ili kukabiliana na mzozo wa DRC.

Wednesday, November 21, 2012

Special Envoy from Gabon delivers Special Message to President Kikwete



H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania welcomes Special Envoy Mr. Serge Mickoto (left), Director General of the Gabonese Strategic Investment Fund. Mr. Mickoto is in the country to deliver a Special Message from H.E. Ali Bongo Ondimba of the Republic of Gabon to President Kikwete.



H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania receiving Special Message from H.E. Ali Bongo Ondimba of the Republic of Gabon, delivered by Special Envoy Mr. Serge Mickoto (left), Director General of the Gabonese Strategic Investment Fund.  (This photo is courtesy of www.issamichuzi.blogspot.com)


President Kikwete in discussion with Mr. Mickoto, Special Envoy from Gabon.


Hon. Bernard K. Membe (MP) (left), Minister of Foreign Affairs and International Co-operation and Ambassador Vincent Kibwana (2nd left), Director of the Department of Africa in the Ministry of Foreign Affairs listen to President Kikwete's discussion with Mr. Mickoto.


President Kikwete (center), in a group photo with Special Envoy from Gabon, Mr. Serge Mickoto (2nd left).  Also in the photo is Hon. Bernard K. Membe (MP) (right), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation.



All other photos are by Tagie Daisy Mwakawago





Newly Designate High Commissioner of Canada presents Letters of Credence


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania (right), awaits the newly designate High Commissioner of Canada to the United Republic of Tanzania to presents his original Letters of Credence before him.  Others in the photo are Hon. Bernard K. Membe (MP) (2nd left), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation and Mrs. Grace Shangali (left), Assistant Director of the Department of Europe and Americas in the Ministry of Foreign Affairs.


President Kikwete receives original Letters of Credence from Ambassador Alexandre Lévêque, new High Commissioner of Canada to Tanzania.  Witnessing the occasion is Mr. Japhet Mwaisupule (2nd right), Acting Chief Protocol.


President Kikwete introduces new High Commissioner of Canada, Ambassador Lévêque to the Minister of Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard K. Membe (MP).  Second left is Mrs. Grace Shangali, Assistant Director of the Department of Europe and Americas in the Ministry and Mr. Grayson Ishengoma (left), Desk Officer of Canada at the Ministry.


President Kikwete in discussion with Ambassador Lévêque, High Commissioner of Canada to the United Republic of Tanzania.


Hon. Minister Membe listen keenly to President Kikwete (not in the photo) during his discussion with Ambassador Alexandre Lévêque, the new High Commissioner of Canada to Tanzania.  Right is Mrs. Grace Shangali, Assistant Director of the Department of Europe and Americas in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.



All photos by Tagie Daisy Mwakawago



Newly Designate Ambassador of Iran to Tanzania presents his Credence



H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania waits for the newly designate Ambassador of the Islamic Republic of Iran to the United Republic of Tanzania, H.E. Mehdi Agha Jafari to presents his Letters of Credence before him today at the State House in Dar es Salaam.  Others in the photo are Hon. Bernard K. Membe (MP) (3rd left), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Ambassador Simba Yahyra (2nd left), Director of the Department of Middle East at the Ministry and Mr. Christopher Mvula (left), Assistant Director of the Deparment of Middle East at the Ministry.


H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete receives original Letters of Credence from newly designate Ambassador of the Islamic Republic of Iran, H.E. Mehdi Agha Jafari.  


President Kikwete introduces Ambassador Jafari to Hon. Membe.


President Kikwete in discussion with Ambassador Jafari.


Hon. Membe (left), Ambassador Yahya (center), and Mr. Mvula (right), keenly listening to the discussion between President Kikwete and Ambassador Jafari (both not in the photo). 


All photos by Tagie Daisy Mwakawago