Friday, November 16, 2012

Tanzania na Malawi zaendelea na majadiliano kuhusu Ziwa Nyasa

 Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. John Haule kufungua kikao cha Pamoja  cha Maafisa Waandamizi kutoka Tanzania na Malawi kuendelea na majadiliano kuhusu mgogoro wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa. Majadiliano hayo yanafanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (mwenye kipaza sauti) akisoma agenda za kikao hicho wakati wa majadiliano. Wengine katika picha ni Mhe. Patrick Tsere (kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Balozi Kasyanju (kulia) na wajumbe wengine kutoka Tanzania.
Wajumbe kutoka Malawi wakimsikiliza Bw. Haule (hayupo pichani) wakati wa majadiliano hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Malawi, Bw. Patrick Kabambe (wa tatu kutoka kushoto) akichangia maoni yake wakati wa majadiliano hayo. Wengine katika picha ni wajumbe aliofuatana nao kutoka Malawi.
Wajumbe kutoka Tanzania wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Malawi (hayupo pichani) wakati wa majadiliano hayo.
Wajumbe wa pande zote mbili wakati wa majadiliano hayo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.