Wednesday, January 31, 2018

Ban Ki-moon ashiriki kwenye ufunguzi wa Ubalozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea

Picha ya pamoja baada ya Mawaziri wa Tanzania na Korea Kusini kukata utepe na kuzindua rasmi majengo ya Ubalozi wa Tanzania tarehe 31 Januari, 2018. Kutoka kushoto ni Bw. Park Young min, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Afrika; Mhe. Silvester Bile, Kiongozi wa Mabalozi wa Afrika na Balozi wa Ivory Coast; Mhe. Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mstaafu; Mhe. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje Tanzania; Mhe. Lim Sung-nam, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Korea Kusini; Mhe. Matilda Masuka, Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini; na Mhe. Salim Alharthy, Kiongozi wa Mabalozi na Balozi wa Falme ya Oman nchini Korea ya Kusini.  

Mheshimiwa Matilda Masuka (kushoto) Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea akiwakaribisha na kuwashukuru wageni waalikwa waliohudhuria kwa wingi kwenye ufunguzi rasmi wa Ofisi za Ubalozi tarehe 31 Januari 2018. Awali Tanzania ilikuwa inawakilishwa nchini humo kutokea Japan. Mheshimiwa Balozi Matilda Masuka aliteuliwa Desemba 3, 2016 na baadaye kuapishwa kuwa Balozi wa kwanza mwenye makazi yake Mji Mkuu wa Seoul, Jamhuri ya Korea. Anayeangalia (kulia) ni mfanyakazi wa Ubalozini Debora Mikwenda.  

Mheshimiwa Lim Sung-nam, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea akizungumza kwa niaba ya Serikali yake wakati wa ufunguzi rasmi wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo. Kwenye salamu zake za ufunguzi, Mheshimiwa Sung-nam amesifu jitihada za Serikali ya Tanzania kukuza uchumi na kusifu ushawishi na karisma ya Balozi Masuka ambayo imewezesha kuvutia Mabalozi na wanadiplomasia wengi Jijini Seoul kushuhudia ufunguzi wa ofisi za Ubalozi. 

Mheshimiwa Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mstaafu akihutubia wageni waliofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Tanzania. Mheshimiwa Ki-moon, ambaye alitambulishwa kama rafiki mkuu wa Tanzania nchini humo, alipongeza Serikali ya Tanzania kwa kufanikiwa kusimika bendera ya Tanzania nchini mwake baada ya miaka 25 ya uhusiano mzuri wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi. 


Viongozi wakikata utepe


Kibao cha uzinduzi kikifunguliwa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Jamhuri ya Korea kwa pamoja. 

Juu ni picha ya pamoja ya Mabalozi wanawake wenye makazi yao Seoul na chini ni Mabalozi wa nchi za Kiafrika wenye makazi yao Seoul. 


Jumuiya ya Wanafunzi wa Kitanzania (diaspora) walioshiriki kikamilifu katika uzinduzi wa ofisi hizo, walitumbuiza kwa kuimba nyimbo mbalimbali za Kitanzania na kucheza muziki wa dansi wa Kitanzania. 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.