Saturday, January 20, 2018

Wizara yawanoa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki

   Balozi Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifungua Semina Elekezi kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki iliyofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018.

Wajumbe wa Semina hiyo wakimsikiliza Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa ufunguzi wa Semina ya siku mbili ya kuwaongezea uwezo Wabunge wa Tanzania watakaowakilisha nchi kwenye Bunge la Nne la Afrika Mashariki.

Dkt. Suzan Kolimba, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwatambulisha baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara hiyo kwa Wabunge wa Tanzania wa Bunge la Afrika Mashariki wakati wa Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya Wabunge hao. 

   Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki. Kulia kwa Waziri Mahiga ni Mwenyekiti wa Wabunge hao Mhe. Dkt. Abdullah Makame. Wengine waliosimama kutoka kushoto ni Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe, Mhe. Happiness Lugiko, Mhe. Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa, Mhe. Pamela Maasay na Mhe. Adam Kimbisa.

Waheshimiwa Dkt. Mahiga na Dkt. Kolimba kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi na maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Nne la Afrika Mashariki kwenye Semina elekezi iliyoandaliwa na Wizara kwa lengo la kuwaongezea uzoefu Wabunge hao. 

Mheshimiwa Adam Kimbisa akisalimiana na Mheshimiwa Dkt. Mahiga wakati wa Semina hiyo ya siku mbili iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 19-20 Januari, 2018. 

Mheshimiwa Pamela Maasay akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. 


Mheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki
Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. Wengine kwenye picha waliokaa kuanzia kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Idara Kuu ya Usalama wa Taifa  Dkt. Modestus Kapilimba, Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa Wizara na Balozi Ramadhan Mwinyi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara.


Mheshimiwa Mhandisi Mohamed Habib Mnyaa akijitambulisha wakati wa Semina elekezi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki



Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Valentino Mlowola akitoa mada kuhusu mapambano ya rushwa wakati wa Semina elekezi kwa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki. Kabla ya mada hiyo Mkurugenzi Dkt. Kapilimba wa Idara Kuu ya Usalama wwa Mataifa alitoa mada kuhusu uzalendo na usalama wa nchi.

Mheshimiwa Adam Kimbisa akichangia hoja kuhusu mapambano ya rushwa nchini iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa TAKUKURU Bw. Valentino Mlowola wakati  wa Semina elekezi kwa Wabunge wa Afrika Mashariki iliyoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Dkt. Benard Achiula, Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia akiwasilisha mada kuhusu itifaki na diplomasia wakati wa Semina hiyo. Pichani Dkt. Achiula akiwa na sahani na vyombo vya kulia chakula akionesha mfano wa kula kwenye dhifa za kitaifa. Mada hiyo iliambatana pia na andiko kuhusu Diplomasia ya Uchumi ambao ndio mwelekeo wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania. 

Jaji (Mstaafu) Harold Nsekela, Kamishna wa Maadili, Ofisi ya Rais - Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma  akitoa mada kuhusu maadili ya Mbunge wa Afrika Mashariki na Taswira ya Nchi katika uwakilishi wa Taifa.

Dkt. Maduka Kessy, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango akitoa mada kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na mipango mbalimbali ya maendeleo kwenye maeneo ya kimkakati katika Mtangamano wa Afrika Mashariki.

Bw. Stephen Mbundi, Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Wizara akichangia mada wakati wa Semina Elekezi ya Wabunge wa Bunge la nne  la Afrika Mashariki.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.