Tuesday, January 30, 2018

Naibu Waziri akutana na Balozi wa Singapore nchini

 Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akizungumza na Balozi wa Singapore nchini Mhe. Balozi Tan Puay Hiang, alipomtembelea Wizarani Jijini Dar es Salaam, tarehe 29/11/2018. 
Katika mazungumzo hayo Mhe. Dkt. Kolimba alishukuru Serikali ya Singapore kwa misaada wanayoitoa kwa Tanzania hasa katika eneo la elimu, Mhe. Dkt Suzan alitumia nafasi hiyo kumwalika Balozi huyo kutembelea vivutio vya utalii vilivyo nchini ikiwa ni pamoja na kuhamasisha Watalii kutoka nchi hiyo kutembelea Tanzania. 
Kwa upande wake Mhe. Puay Hiang aliikaribisha Tanzania kujifunza Singapore hasa katika eneo la Utalii na alimhakikishia Mhe. Waziri kwamba nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali.

Mhe. Dkt Suzan Kolimba na Mhe. Balozi Puay Hiang wakiendelea na mazungumzo, wanaofuatilia ni Bw. Emmanuel Luangisa; Kaimu Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia (Kushoto), Bw. Charles Faini Msaidizi wa Naibu Waziri ( Mwisho kushoto) na Bw. Lucien Hong Mkurugenzi msaidizi kutoka ubalozi wa Singapore ( kulia).    
                                     
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.