Wednesday, January 31, 2018

Kongamano la Biashara la Tanzania na Jamhuri ya Korea katika Picha

Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisalimiana na Bw. Jundong Kim, Makamu Mwenyekiti wa "Korea Chambers of Commerce and Industry" muda mfupi kabla ya uzinduzi wa Kongamano la kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini tarehe 31 Januari 2018.  

Bw. Kim akimuelezea Mheshimiwa Waziri Mahiga na ujumbe wake kwa kifupi kuhusu kazi za KCCI kabla ya kufungua Kongamano la Kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini. 

Mheshimiwa Matilda Masuka, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea akiwakaribisha wajumbe waliofuatana na Mheshimiwa Waziri kwenye ziara hiyo kuingia kwenye ukumbi wa Kongamano.

Watanzania wanaoishi nchini Korea wakiwa kwenye mashati maalum ya kutangaza Kongamano ambao pia walikua wakitoa huduma mbalimbali wakati Kongamano likiendelea.









Pichani juu na chini Mheshimiwa Waziri Mahiga akiagana na Watanzania walioshiriki kwenye Kongamano hilo baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya majadiliano.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.