Monday, January 29, 2018

Mhe. Naibu Waziri amuaga Balozi wa Zimbabwe.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Suzan Kolimba akimkabidhi zawadi Balozi wa Zimbabwe nchini anayemaliza muda wake Mhe. Balozi Edzai Chimonyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika Serena Hotel tarehe 29/01/2018. 

Katika hafla hiyo Mhe. Dkt Suzan alimshukuru kwa ushirikiano mkubwa kwa kipindi chote alichokuwa Balozi hapa nchini na kumtakia heri katika majukumu yake mapya. Mhe. Balozi  alimshukuru Naibu Waziri kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Ushirikiano mkubwa alioupata wakati akitekeleza majukumu yake hapa nchini.

Waheshimiwa Mabalozi, Mhe. Brahim Buseif Balozi wa Sahara Magharibi nchini (wa kwanza kushoto) na Mhe. Benson Keith Chali Balozi wa Zambia Nchini wakifuatilia hafla hiyo

Mhe. Naibu Waziri Dkt Suzan Kolimba akiteta jambo na Mhe. Balozi Edzai Chimonyo katika hafla hiyo.


 Baadhi ya Maafisa kutoka Wizarani Bi. Elizabeth Mutunga na Bi. Robi Bwiru wakifuatilia hafla hiyo.

 Bw.Ayoub Mdeme Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika (Kulia) na Bw. Martin Tavenyika kutoka Ubalozi wa Zimbabwe nchini (kushoto) wakiwa katika hafla hiyo.

Bw. Suleiman Saleh Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika akiteta jambo na Mhe. Thamsanga Dennis Msekelu Balozi wa Afrika Kusini nchini, anayefuatilia ni Mhe. Balozi Edzai Chimonyo.

Maafisa kutoka Wizarani Bw. Charles Faini na Bi. Mercy Kitonga nao wakiwa katika hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.