Tuesday, January 30, 2018

Tanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na Singapore

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akizungumza na Balozi wa Singapore nchini mwenye makazi yake nchini Singapore, Mhe. Tan Puay Hiang alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo yao yalijikita katika kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano pamoja na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara ili kuweza kuinua uchumi wa mataifa hayo.
Mazungumzo yakiendelea.

Mhe. Tan Puay Hiang akimkabidhi Balozi Mwinyi zawadi ya kitabu.

Picha ya pamoja Kaimu Katibu Mkuu, Mhe. Balozi Tan Puay Hiang, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Luhangisa (kulia) na Mkurugenzi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje wa Singapore, Bw. Lucien Hong(kushoto) 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.