Sunday, November 20, 2022

MABALOZI WAHIMIZWA KUBIDHAISHA KISWAHILI

 


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu akizungumzia umuhimu wa wadau wa lugha ya Kiswahili kushirikian katika kutekeleza Mkakati wa kubidhaisha lugha ya Kiswahili wakati wa mkutano wa Mabalozi wa Tanzania uliomalizika Zanzibar tarehe 20 Novemba 2022

Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Bi. Consolata Mushi akiwasilisha mada ya mkakati wa kubidhaisha lugha ya Kiswahili katika mkutano wa Mabalozi wa Tanzania uliomalizika Zanzibar tarehe 20 Novemba 2022

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu akimkabidhi tuzo maalum Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Samwel Shelukindo kwa kutambua mchango wake wa kuipigania lugha ya Kiswahili kwenye medani za kimataifa na kupelekea Unesco kutangaza Julai 7 ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipokea vitabu vya lugha ya Kiswahili kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu kwa ajili ya kutumiwa na Balozi za Tanzania Nje kufundishia lugha ya Kiswahili katika maeneo yao ya uwakilishi 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.