Tuesday, December 11, 2018

Tanzania yazidi kung'ara Maonesho ya Jua Kali/Nguvu Kazi nchini Kenya


Waziri wa Biashara na Viwanda wa Kaunti ya Siaya Kenya Mhe. Jaokon O. Odinga (katikati) akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Balozi Dkt. Pindi Chana (kulia)  alipotembelea banda la Tanzania katika Maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yanayoendelea katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Eldoret nchini Kenya, pembeni ni Mkurugenzi  Kitengo cha Diaspora Balozi Anisa Mbega wa Wizara ya Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Balozi wa Uganda nchini Kenya, Mhe. Phibby Otaala (kushoto) akibadilishana mawazo na Afisa Biashara wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Hassan Mnondwa (aliyesimama) juu ya ubora wa bidhaa za Tanzania zinazozasilishwa  na wajasiriamali  na kuuzwa katika maonesho ya Jua kali/Nguvu Kazi alipotembelea banda la Tanzania. Anayeweka saini kitabu cha wageni ni  Mhe. Namugwanya Benny Bugembe (MP) Waziri wa Nchi anayesimamia Mamlaka ya Jiji la Kampala Uganda.
Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Pindi Chana wa pili kutoka kushoto, Balozi wa Uganda nchini Kenya Mhe. Phibby Otaala wa pili kutoka kulia wakishikana mikono pamoja na viongozi wengine wa Uganda. Kutoka kushoto ni Waziri wa Biashara  na Viwanda wa Kaunti ya Uasin Gishu Dkt. Emily Kongos na kulia ni Mhe. Namugwanya Benny Bugembe (MP) Waziri wa Nchi anayesimamia Mamlaka ya Jiji la Kampala Uganda wakishikana mikono kuonesha ishara ya mshikamano wa viongizi wanawake wa Afrika Mashariki.

Juu na Chini ni Wananchi wa Kaunti ya Uasin Gishu wakitembelea kwa wingi katika mabanda ya Tanzania   wakifurahia na kununua bidhaa zinazozalishwa na Wajasiriamali na kuoneshwa katika maonesho ya Jua Kali/Nguvu Kazi yanayoendelea  mjini Eldoret.
Maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yanayoendelea  kufanyika katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Eldoret Kenya ni ya kwanza kufanyika nje ya miji mikuu ya Nchi Wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.