Tuesday, December 11, 2018

Maonesho ya Jua Kali/Nguvu Kazi yamalizika kwa mafanikio kwa Tanzania


Seneta wa Kaunti ya Uasin Gishu, Mhe. Profesa Magrate Kamar akifunga Maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi jana yaliyofanyika kwa muda wa siku kumi katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Endoret Kenya. Kwenye hotuba yake Prof. Kamar aliwataka wajasiriamali kuongeza mawasiliano miongoni mwao ili kukuza soko la bidhaa zao ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo zimekuwa na viwango bora

 Naibu Katibu wa Wizara ya Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto wa Zanzibar,  Bi. Mau Makame Rajab akitoa neno la shukrani katika sherehe ya kufunga  maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi jana zilizofanyika katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Eldoret, Kenya.
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Hassan Mnondwa akipokea cheti cha pongezi jana kwa mchango wake wa kufanikisha kufanyika kwa maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yaliyofanyika katika kaunti ya Uasin Gishu, Eldoret nchini Kenya

Afisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi na Ajira, Bi. Sara Daudi akipokea cheti cha pongezi jana  kwa mchango wake wa kufanikisha kufanyika kwa maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yaliyofanyika katika kaunti ya Uasin Gishu, Eldoret.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.