Monday, November 19, 2018

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa Namibia nchini



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi akisalimiana na Balozi wa Namibia nchini, Mhe. Theresa Samaria alipofika Wizarani kwa ajili ya kumsalimia na  kuzungumzia kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia kwenye sekta mbalimbali ikiwemo biashara, kilimo, uvuvi na mifugo. Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 19 Novemba, 2018.
Mhe. Balozi Samaria akimweleza Dkt. Kasidi kuhusu fursa mbalimbali za biashara ambazo Tanzania inaweza kuzichangamkia kwenye nchi yake ambayo ina ukame uliokithiri kutokana na kuzungukwa na Majangwa ya Kalahari na Namib. Fursa hizo ni pamoja na biashara ya nyama, matunda, nafaka mbalimbali na korosho.
Mazungumzo yakiendelea huku Afisa aliefuatana na Balozi Samaria akinukuu
Katibu Mkuu, Dkt. Kasidi akisoma nyaraka aliyopatiwa na Balozi Samaria ambayo ni mkataba ulioanzisha Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Namibia miaka 20 iliyopita. 

Dkt. Kasidi akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi Samaria mara baada ya kumaliza mazungumzo yao


Piacha ya pamoja kati ya Dkt. Kasidi na Balozi Samaria pamoja na  Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Ubalozi wa Namibia nchini walioshiriki mazungumzo kati ya viongozi hao 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.