Friday, October 15, 2021

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI ATETA NA BALOZI WA CHINA HAPA NCHINI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) aakiwa katika mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Balozi Chen Mingjian.

Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amekumbushia utekelezwaji wa ahadi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi ya kuipa Tanzania masoko ya bidhaa za asali na mabondo, ahadi aliyoitoa Chato Mkoani Geita mwezi Januari,2021 wakati wa ziara yake hapa nchini


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China hapa Nchini Balozi Chen Mingjian mara baada ya kumaliza mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.