Saturday, October 2, 2021

WAZIRI MULAMULA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA NIGERIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameshiriki sherehe ya Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Taifa hilo iliyoandaliwa na Ubalozi wa Nigeria hapa nchini. 

Sherehe za Maadhimisho hayo ambazo zimefanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam zimehudhuriwa na wawakilishi kutoka makundi mbalimbali katika jamii ikiwemo, Wafanyabiashara, Wanadiplomasia, Watendaji na Viongozi kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali. 

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho hayo Waziri Mulamula licha ya kuipongeza Serikali ya Shirikisho la Nigeria kwa kuendelea kulinda Uhuru wake na kudumisha amani na usalama pia, amepongeza hatua ya maendeleo ya kiuchumi iliyofikiwa na Taifa hilo chini ya uongozi mahiri wa Rais Mhe. Muhammadu Buhari. Aliongeza kusema kwa kutambua hilo Tanzania itaendelea kudumisha na kukuza mahusiano ya kidiplomasia na kibiashara na Nigeria ili kwa pamoja kuweza kunufaika kiuchumi kutokana na fursa zilizopo. 

Kwa upande wake Balozi wa Nigeria hapa nchini Mhe. Hamisu Takalmawa amesema Serikali ya Shirikisho la Nigeria itaendelea kutumia matunda ya Uhuru wake kwa kuchukua hatua stahiki za kuboresha na kukuza mahusiano mazuri ya Kidiplomasia yaliyopo baina yake na Mataifa mengine ulimwenguni. 

Nigeria ilipata Uhuru wake Oktoba 1, 1960
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akifurahia jambo kwenye sherehe za Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Nigeria zilizofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akihutubia katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Nigeria zilizofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Mhe. Hamisu Takalmawa akihutubia kwenye sherehe za Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Nigeria zilizofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Mhe. Hamisu Takalmawa (kulia) na Balozi wa Comoro hapa nchini Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed Fakih (kushoto) wakikata keki kwenye sherehe za Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Nigeria
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akihutubia katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Nigeria zilizofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja Wanadiplomasia walioshiriki katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Nigeria
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Mhe. Hamisu Takalmawa (kulia) na Balozi wa Comoro hapa nchini Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed Fakih (kushoto) wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakiendelea kwenye sherehe za Maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Nigeria

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.