Thursday, April 18, 2019

Fursa ya Ajira.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NAFASI YA AJIRA KATIKA SEKRETARIETI YA JUMUIYA YA UKANDA WA MAZIWA MAKUU (ICGLR).

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inawahamasisha Watanzania wenye sifa, kuomba nafasi ya ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR).

Ajira hiyo ni Mtaalam wa Uhakiki wa Nyaraka. Taarifa zote muhimu kuhusu fursa hiyo ya ajira zinapatikana kwa kupitia tovuti www.icglr.org.

Maombi yote yatumwe kwenda katika barua pepe jobs@icglr.org na nakala itumwe katika barua pepe gerard.nayuburundi@icglr.org  yakiwa na kichwa cha habari Maombi ya nafasi ya Mtaalam wa Uhakiki wa Nyaraka.

Mwisho wa kutuma maombi kwa nafasi hiyo ni  tarehe 25 Aprili, 2019.

    Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
      Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.