Friday, April 12, 2019

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Mtaalam wa Uchumi kutoka Ujerumani


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kikao na Prof. Helmut Asche (kulia) ambaye ni Mtaalam wa Uchumi hususan masuala yanayohusiana na Ubia wa Kiuchumi kati ya Ulaya na Afrika (EPA) kutoka Ujerumani. Kikao hicho kilifanyika hivi karibuni jijini Dodoma.
Prof. Asche kutoka Ujerumani akizungumza kwenye kikao kati yake na Naibu Waziri, Mhe. Ndumbaro. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akimsikiliza Prof. Asche. 
Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Prof. Asche akifafanua jambo kuhusu EPA wakati wa kikao kati yake na Mhe. Dkt. Ndumbaro huku wajumbe wengine wakifuatilia. Kulia ni  Bw. Jestas Nyamanga, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Dkt. Mnyepe (kulia) akiwa na Dkt. Edwin Mhede (katikati), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wakifuatilia kikao. 
Kikao kikiendelea
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiteta jambo na Prof. Asche mara baada ya mazungumzo kati yao
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiwa na Prof. Asche na wajumbe wengine wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima ya Prof. Asche.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.