Wednesday, April 24, 2019

Nafasi za Ajira Katika Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali


Dodoma, 24 Aprili 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Nafasi za Ajira

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuwahimiza Watanzania wenye sifa kuomba fursa ya ajira iliyotangazwa na Sekretarieti ya Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali (Organization for the Prohibition of Chemicals Weapons-OPCW) iliyopo The Hague, Uholanzi. Nafasi hiyo ni ya Technical Support Officer-P3 ambapo mwisho wa kufanya maombi ni tarehe 06 Juni 2019.

Wenye sifa zinazohitajika, wanashauriwa kufanya maombi kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya sekretarieti; www.opcw.org

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.