Tuesday, April 16, 2024

NJE SPORT YAIZIBUA BILA HURUMA MAMLAKA YA AFYA YA MIMEA NA VIUATILIFU

Timu ya Nje – Sport wanaume imeizibua bila huruma magoli 2 kwa buyu Timu ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) katika mchezo uliofanyika kwenye  viwanja vya Shule ya sekondari ya Iliboru jijini Arusha leo Aprili 16, 2024.

Magoli hayo yamepachikwa wavuni na washambuliaji hatari wa timu hiyo, Bw. Mikidadi Magola, Goli la kwanza na goli la pili likiwekwa kimyani kwa ustadi mkubwa na Bw. Mukrimu Mustafa. 

Kocha wa timu hiyo, Bw. Shabani Maganga aliwapongeza wachezaji wake kwa kufuata maelekezo yake pamoja na kucheza vizuri na kuifanya timu yake kubeba alama tatu muhimu katika mzunguko wa kwanza

Katika mchezo mwingine timu ya Wanawake ya mpira wa pete ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (Nje Sports) imepokea kichapo cha magoli 52 kwa 7 kutoka  timu ya Ikulu. 

Mmoja wa wachezaji wa timu hiyo, Bi. Pili Sukwa ameeleza kuwa licha ya kichapo hicho, Timu yake imeendelea kuimarika na ameahidi kufanya vizuri katika michezo inayofuata.

 Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wameungana na mamia ya watumishi wenzao kushiriki michezo ya Mei mosi ambapo maadhimisho ya kitaifa yamepangwa kufanyika Mkoani Arusha.

Timu ya mpira wa Miguu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla kuingia uwanjani kucheza dhidi ya Timu ya Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA)

Timu ya Mpira wa Miguu ikifanya mazoezi ya kupasha viungo.



Mechi kati ya Nje na Hazina FC ikiendelea katika uwanja wa Ujenzi mjini Morogoro

Mshambuliaji machachari wa Nje Sports Bw. Mukrimu Mustafa akipongezwa na kocha wa Nje FC katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Ilboru mjini Arusha


Kepteni wa Nje FC akipatiwa matibabu mara baada ya kuchezewa rafu na mchezaji wa timu pinzani.

Wachezaji wa Nje FC wakiburudika mara baada ya kupata ushindi wa 2 - 0.

Timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na Timu ya Ikulu muda mfupi kabla kuingia uwanjani kucheza mchezo wa raundi ya kwanza.

Timu ya mpira wa pete ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipasha viungo muda mfupi kabla kuingia uwanjani kucheza dhidi ya Timu ya Ikulu


Juu na chini Mchezo ukiendelea.




 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.