Wednesday, April 3, 2024

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA BALOZI WA HESHIMA WA TANZANIA NCHINI DENMARK

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (Mb) akizungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania Nchini Denmark Bw. Simon Mears hayupo pichani walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Grace Olotu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania Nchini Denmark Bw. Simon Mears (wa kwanza Kushoto)  walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, wa pili kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Grace Olotu na wa kwanza kulia Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Swahiba Mndeme.

mazungumzo yakiendelea

 Balozi wa Heshima wa Tanzania Nchini Denmark Bw. Simon Mears akizungumza kitu alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba hayupo pichani katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, anayesikiliza kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Grace Olotu.

 

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (Mb) amekutana na kuzungumza na Balozi wa Heshima wa Tanzania Nchini Denmark Bw. Simon Mears katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katıka mazungumzo na Bw. Mears Mhe. Waziri Makamba amempongeza kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya nchini Denmark kwa niaba ya Tanzania

Amemwambia kuwa Serikali ya Tanzania iko tayari kumpa ushirikiano utakaomuwezesha kutekeleza majukumu yake nchini Denmark.

Amesema Tanzania sasa inaangalia namna bora ya kufanya biashara na Denmark ili kuvutia Wafanyabiashara na wawekezaji wengi zaidi nchini.

Amesema  Serikali inachukua hatua kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini ili kuvutia wawekezaji hivyo fursa hiyo itumiwe kikamilifu.

Naye Bw. Mears ameshukuru kukutana na mhe Waziri  na kuahidi kuendelea kufanyakazi aliyokabidhiwa kwa ufanisi .

Amesema Denmark ina nia ya kuendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo ya nishati ya kijani, nishati mbadala pamoja na usalama.

Tanzania na Denmark zimekuwa zikishirikiana katika maeneo ya biashara, uwekezaji, utalii, elimu na etc

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.