Friday, October 24, 2014

President Kikwete accorderd rousing Karibu, as China's President Xi Jinping formaly welcomes him to Beijing

President Xi Jinping of China welcomes President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete to the Great Hall of the People in Beijing this evening during the official formal reception at the climax of the State visit at the invitation of the Chinise Leader
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and the First Lady Mama salma Kikwete pose for an official photograph with their  host China's President Xi Jinping and his wife China's First Lady Peng Liyuan shortly after they arrived for an official formal reception at the Great Hall of the People in Beijing this evening

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and his host Chinese President Xi Jinping inspects a guard of honor mounted China's People Defense force in Beijing this evening during a formal reception at the Great Hall of the people. President Kikwete is on a State Visit to China invitation of  President Xi Jinping.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and his host President Xi Jinping waves to the cheering crowd during a formal reception for the President and his delegation held at the Great Hall of  the People in Beijing at the climax of his State visit today 
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete introduces former OAU/AU Secretary General Salim Ahmed Salim to China's President Xi Jinping during the formal reception held at the Great Hall of the People in Beijing this evening Left is the Minister for Foreign Affairs Mr Bernard Membe and second left is CCM Secretary General Abdulrahman Kinona.





==========================================================================

China ya yamwaga neema kubwa kwa Tanzania

Jamhuri ya Watu wa China leo, Ijumaa, Oktoba 24, 2014, imetangaza neema kubwa kwa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kutoa dola za Marekani milioni 85 kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kusaidia Tanzania kufanya mageuzi ya viwanda.

Neema hiyo kwa China kwa Tanzania imetangazwa na Rais Xi Jinping wa nchi hiyo katika mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati yake na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye yuko katika ziara rasmi ya siku sita katika China

Mazungumzo hayo kwenye jumba la The Great Hall of the People yamefanyika baada ya Rais Kikwete kukaribishwa rasmi katika Jamhuri ya Watu wa China kwa kupokelewa na Rais Xi Jinping katika eneo la East Plaza ya Jumba hilo.

Katika mapokezi hayo yakuvutia na kusisimua, Rais Kikwete amepigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride la ukakamavu la Jeshi la Ukombozi la Wananchi wa China la People's Liberation Army.
Katika mazungumzo hayo, Rais Xi Jinping alitangaza kuwa China itaipatia Tanzania kiasi cha dola milioni 85 ikiwa ni mchanganyiko wa msaada na mkopo usiokuwa na riba, fedha ambazo Tanzania itaamua yenyewe jinsi gani yakuzituma.

"Katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania kuboresha maisha ya wananchi wake, napenda kutangaza kuwa Jamhuri ya watu wa China itatoa kiasi cha RMB milioni 200 ikiwa ni msaada na RMB 200  milioni nyingine zikiwa ni mkopo ni mkopo usio kuwa na riba kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kiasi cha RMB 100 milioni za msaada kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambazo zitatumika kwa kadri Serikali hizo mbili zitakavyoamua,'' amesema Rais Jinping.

Rais huyo wa China pia ametangaza kuwa nchi hiyo itaisaidia Tanzania katika uendelezaji wa maeneo ya uwekezaji ya EPZ, uendelezaji wa miundombinu itaharakisha ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo na itaingia katika shughuli za kutafuta gesi na mafuta katika ukanda wa Bandari ya Hindi katika eneo la Tanzania.

Rais Jinping pia ametangaza kuwa Serikali ya China imefanya uamuzi wa kuikarabati Reli ya Uhuru ya TAZARA inayounganisha Tanzania na Zambia na yenye urefu wa Kilometa 1,860 na kusaidia uendeshaji wa reli hiyo. "Ili kutekeleza uamuzi huu kwa haraka, napendekeza kuundwa kwa kamati ya pamoja ya wataalam kuandaa ramani ya namna ya kuitoa reli hiyo katika matatizo yake ya sasa.''

Rais Jinping ametangaza kuwa Serikali yake itatoa nafasi 100 za masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi kutoka Tanzania katika miaka mitano ijayo, itaongeza idadi ya madaktari ambao China inapeleka Tanzania, itahimiza makampuni zaidi ya China kuwekeza katika Uchumi wa Tanzania na kuzishawishi taasisi za kifedha za China kuanzisha shughuli zake katika Tanzania.

Kiongozi huyo wa China pia ametangaza kuwa nchi yake itajenga Chuo kikubwa cha mafunzo ya ufundi katika Tanzania na itaendeleza kushirikiana na Tanzania katika eneo la uimarishaji wa ulinzi na usalama.

Rais Jinping amesema kuwa urafiki na uhusiano kati ya China na Tanzania ni mfano unaong'ara wa uhusiano mzuri na mwema duniani na kuwa china iko tayari kutoa uzoefu wake wa maendeleo kwa Tanzania bila wasiwasi wowote.

Rais Kikwete amemshukuru sana Rais Jinping na Jamhuri ya watu wa China kwa misaada yake ambayo baadhi yake haikutarajiwa.

Imetolewa na: 
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikuli - Dar es salaam     

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.