Monday, October 13, 2014

Naibu Waziri akutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa DRC

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Celestin Tunda ya Kasende alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu masuala ya ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. Katika mazungumzo hayo Mhe. Tunda ya Kasende aliishukuru Serikali ya Tanzania na Watanzania kwa ujumla kwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha amani inarejea DRC. Mhe. Tunda ya Kasende pamoja na ujumbe wake  yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Rose Kitandula (kushoto) akiwa na Bw. Adam Isara, Msaidizi wa Naibu Waziri na Bi. Eva Ng'itu wakifuatilia mazungumzo ya Naibu Mawaziri wa Tanzania na DRC (hawapo pichani)
Mhe. Dkt. Maalim akimweleza jambo Mhe. Tunda ya Kasende wakati wa mazungumzo yao.
Sehemu ya ujumbe uliofuatana na Mhe. Tunda ya Kasende wakifuatilia mazungumzo. Kulia ni Dkt. Jean Marie Okwo Bele ambaye ni Mkurugenzi wa Chanjo katika Shirika la Afya Duniani (WHO)
Mazungumzo yakiendelea
Dkt. Maalim akiagana na Mhe. Tunda ya Kasende mara baada ya mazungumzo yao.

Picha na Reginald Philip















No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.