Wednesday, October 1, 2014

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Rais Kikwete ateua Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Bw. Jack Mugendi Zoka kuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada.

Bw. Zoka anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Alex Masinda, ambaye amestaafu kwa mujibu wa sheria.

Kabla ya uteuzi huu, Bw. Zoka alikuwa Ofisa Mwandamizi Ofisi ya Rais, Ikulu.

IMETOLEWA NA KATIBU MKUU, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, Dar es Salaam.

Tarehe 30 Septemba 2014

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.