Saturday, September 5, 2015

Diaspora wahimizwa kuchocheas Maendeleo, Balozi Mulamula


Watanzania wanaoishi ughaibuni (diaspora) wametakiwa kuwa kichocheo cha kuleta maendeleo ya biashara na uwekezaji katika nchi yao ili kuongeza pato la taifa na kuboresha maisha ya mwananchi wa kawaida. Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakati wa kufungua kongamano la wafanyabiashara linalofanyika Birmingham, Uingereza tarehe 4 na 5 Septemba 2015.

Aliwaasa washiriki wa kongamano hilo kulitumia kama jukwaa la kufanya majadiliano kwa madhumuni ya kubadilishana mawazo mapya ili kuibua fursa lukuki za uwekezaji nchini Tanzania. Aidha, aliwahimizawanadiaspora kushirikiana na wajasiliamali wa nyumbani ili kuzitumia fursa hizo ipasavyo.






































 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Peter Kallaghe


Balozi Mulamula aliwahakikishia wnadiaspora waliohudhuria kongamano hilo, kuwa Serikali ina dhamira ya dhati ya kuwashirikisha Watanzania wanaoishi ughaibuni ili kuchangia maendeleo ya nchi yao. Hivyo, aliwahimiza kuja kuwekeza nyumbani kwa kuwa Serikali inajitahidi kuboresha mazingira ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu wa kuwapatia ardhi kwa ajili ya kujenga makazi au kuwekeza.
Aliwaomba wanadiaspora hao, kuwa mabalozi wazuri wa nchi yao kwa kuzitangaza vema fursa zinazopatikana nchini katika sekta mbalimbali kama vile kilimo, miundombinu, nishati, maji, utalii na elimu.


 Bw. David Smith


Akizungumza katika kongamano hilo, Bw. David Smith ambaye alikuwa mmoja wa watoa mada aliwahimiza wanadiaspora kufungua biashara kwa wingi katika nchi zao ili kuondoa tatizo la ukosefu wa ajira. Alisema kuwa hakuna taasisi yenye uwezo wa kuajiri maelfu ya watu. Isipokuwa uanzishaji wa biashara nyingi kunapelekea maelfu ya watu kupata ajira.


 Balozi Mulamula wa katikati kushoto akipokea maelezo ya namna mashine ya kuzalisha vifaa vya ujenzi inavyofanya kazi.

Wakati wa kongamano hilo, Balozi Mulamula alipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya bidhaa na teknojia mbalimbali. Baadhi ya bidhaa na teknolojia alizojionea ni pamoja na   mashine inayotumika kutengeneza aina tofauti za vifaa vya ujenzi kama vigae, matofali na malumalu.  Kampuni ya wanadiaspora ijulikanayo Tanzania Birmingham Ltd inauza machine hizo nchini Tanzania na pia inatumia teknolojia rahisi kujenga nyumba za kisasa kwa gharama nafuu kabisa na kwa muda mfupi. Mmoja wa wafanyakazi wa kmpuni hiyo alisema kuwa teknolojia hiyo imekuwa sio tu mkombozi kwa Watanzania, bali imeondoa tatizo la wanadiaspora wengi ambao walikuwa wanadhulumiwa walipokuwa wanatuma fedha kwa jamaa zao wa karibu ili wawajengee nyumba.



Taasisi mbalimbali za Tanzania zikiwemo Mamlaka ya Bandari Tanzania, ZIPA, ZSSF, Idara ya Uhamiaji, Benki Kuu ya Tanzania ambazo baadhi yao zina huduma maalum kwa ajili ya wanadiaspora zinashiriki kongamano hilo. Aidha, baadhi ya wajasilimali kutoka Tanzania akiwemo Bw. Graison Mutembi anayejishughulisha na uuzaji wa bidhaa za utamaduni kama vinyago anashiriki kongamano hilo sambamba na kuuza bidhaa zake.

Baadhi ya maafisa wa Wizara ya Mambo Nje na wanadiaspora katika kongamano hilo

Na. Ally Kondo, Birmingham

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.