Thursday, September 17, 2015

Balozi Mulamula akutana na Balozi wa Uturuki nchini

 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Uturuki hapa nchini, Mhe. Yasemin Eralp, baada ya Balozi huyo kumtembelea Katibu Mkuu kwa mazungumzo ya kuimarisha uhusiano wa nchi hizi mbili. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 17 Septemba, 2015.
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia mazungumzo hayo. Kulia ni Bw. Kondo Ally na Bw. Anthony Mtafya (kushoto).
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Uturuki hapa nchini Mhe. Yasemin Eralp mara baada ya mazungumzo.
======================================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.