Tuesday, September 8, 2015

Mabalozi Wateule Watatu Wawasilisha Nakala za Hati za Utambulisho.

Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Sweden.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Sweden hapa Nchini Mhe.Katarina Rangnitt, baada ya Balozi huyo kuwasilisha nakala hizo ofisini kwa Waziri Membe leo 08-09-2015.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), akizungumza na Balozi Mteule wa Sweden hapa Nchini Mhe. Katarina Rangnitt, baada ya Balozi huyo kuwasilisha nakala za hati zake ofisini kwa Waziri leo.
Baadhi ya Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, na Msaidizi wa Balozi Mteule wa Sweden, wakifuatilia mazungumzo hayo.

 Mhe. Waziri Bernard Membe (Mb), akifurahia jambo na Balozi Mteule wa Sweden hapa Nchini Mhe.Katarina Rangnitt, baada ya Balozi huyo kuwasilisha nakala zake ofisini kwa Waziri leo.
==============================
Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Finland.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Finland hapa Nchini Mhe.Pekka Hukka, baada ya Balozi huyo kuwasilisha nakala hizo ofisini kwa Waziri leo 08-09-2015.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), akizungumza na Balozi Mteule wa Finland hapa Nchini Mhe.Pekka Hukka, baada ya Balozi huyo kuwasilisha hati zake ofisini kwa Waziri leo.
Balozi Mteule wa Finland hapa Nchini Mhe.Pekka Hukka, akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), baada ya kuwasilisha Nakala za Hati zake za Utambulisho ofisini kwa Waziri leo 08-09-2015.

Baadhi ya Maofisa wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, na Msaidizi wa Balozi Mteule wa Finland wakifuatilia mazungumzo hayo.
====================
Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Uturuki.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb), akisalimiana na Balozi Mteule wa Uturuki hapa Nchini Mhe.Yasemin Eralp, baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala za Hati zake za Utambulisho.
Mhe. Waziri Bernard Membe (Mb.), akizungumza na Balozi Mteule wa Uturuki hapa Nchini Mhe.Yasemin Eralp, ofisini kwake muda mfupi baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala za Hati zake za Utambulisho.
Balozi Mteule wa Uturuki hapa Nchini Mhe.Yasemin Eralp, akisisitiza jambo kwa Mhe. Waziri Bernard Membe, baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala za Hati zake za Utambulisho kwa Mheshimiwa Waziri.
Baadhi ya Maofisa wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, wakifuatilia mazungumzo hayo.
=======================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.