Saturday, September 12, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI  
Taarifa ya kuanguka Msikiti Makhah-Saudi Arabia, Watanzania Salama.

Kufuatia mvua  ilioambatana na upepo mkali na kusababisha kuanguka kwa mashine ya ujenzi wa upanuzi wa eneo la Tawaf ulipo msikiti wa Makkah, msikiti huo umeanguka na kusababisha vifo vya mahujaji.  

Kwa mujibu wa Televisheni ya Saudi Arabia, Saudi TV hadi sasa watu 107 wamefariki dunia na wengine takriban 200 wamejeruhiwa. 

Kufuatia ajali hiyo, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kupitia Ofisi za Ubalozi Riyadh unathibitihsa kuwa Mahujaji wa Tanzania wameanza kuwasili Jeddah kuelekea Makkah leo tarehe 12 Septemba 2015 wakitokea Madina. Hadi sasa Wizara haijapokea taarifa ya Watanzania waliopoteza maisha wala kujeruhiwa kwenye ajali hiyo.
MWISHO.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,

12 Septemba, 2015



 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.