Wednesday, September 9, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Mabalozi kutoka Uswisi, Uturuki, Finland na Sweden

.........Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Uswis
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Uswis hapa nchini Mhe. Florence Tinguely Mattli, katika hafla iliyofanyika leo 09-09-2015, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Uswis hapa nchini Mhe. Florence Tinguely Mattli (wa pili kushoto), pamoja na mumewe ambaye ni balozi mteule wa nchi hiyo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki, na afisa mwandamizi ( wa kwanza kushoto) walioambatana naye kuwasilisha hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
Balozi mpya wa Uswis hapa nchini Mhe. Florence Tinguely Mattli, akisaini kitabu cha wageni ikulu, katika hafla fupi ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais akifanya mazungumzo na Balozi mpya wa Uswis na ujumbe wake, baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), (wa kwanza kushoto) Bi. Tunsume Mwangolombe, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Marekani, na Mshauri wa Rais masuala ya Diplomasia Balozi Samuel Shelukindo wakifuatilia mazungumzo.
Mhe. Florence Tinguely Mattli, Balozi mpya wa Uswis hapa nchini akisikiliza wimbo wa taifa lake muda mfupi baada ya kuwasili ikulu jijini Dar es Salaam.
====================
 .........Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Uturuki.
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Uturuki hapa nchini Mhe. Yasemin Eralp, katika hafla iliyofanyika leo 09-09-2015, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Kikwete akimtambulisha Mhe. Yasemin Eralp.

Mheshimiwa Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Uturuki hapa nchini Mhe. Yasemin Eralp (wa pili kushoto), Maofisa waandamizi kutoka Ubalozi wa Uturuki nchini Tanzania, pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb), katika picha ya pamoja.
Rais akifanya mazungumzo na Balozi mpya wa Uturuki na ujumbe wake, baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.
Mshauri wa Rais masuala ya Diplomasia Balozi Shelukindo (katikati) Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (kulia) na Bi. Tunsume Mwangolombe, wakifuatilia mazungumzo ya Mhe. Rais na Balozi mpya wa Uturuki (hawapo pichani).
Balozi mpya wa Uturuki hapa nchini Mhe. Yasemin Eralp, akisaini kitabu cha wageni Ikulu, katika hafla fupi ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
 Mhe. Yasemin Eralp , Balozi mpya wa Uturuki hapa nchini akisikiliza wimbo wa taifa lake muda mfupi baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
=================
.........Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Finland
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Finland hapa nchini Mhe. Pekka Hukka, katika hafla iliyofanyika leo 09-09-2015, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Balozi mpya wa Finland hapa nchini Mhe. Pekka Hukka, akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.), katika hafla hiyo.

Balozi mpya wa Finland hapa nchini Mhe. Pekka Hukka, akisalimiana na Bi. Tunsume Mwangolombe Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Marekani, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 



Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Finland hapa nchini Mhe. Pekka Hukka.

Rais akifanya mazungumzo na Balozi mpya wa Finland na ujumbe wake, baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.
        Balozi mpya wa Finland hapa nchini Mhe. Pekka Hukka, akisaini kitabu cha wageni ikulu, katika hafla fupi ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.
                                =================
.............Hati za Utambulisho za Balozi mpya wa Sweden.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Sweden hapa nchini Mhe. Katarina Rangnitt, katika hafla iliyofanyika leo 09-09-2015, ikulu jijini Dar es Salaam.

Balozi mpya wa Sweden hapa nchini Mhe. Katarina Rangnitt,akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga wakati wa hafla hiyo.
Mheshimiwa Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Sweden hapa nchini Mhe. Katarina Rangnitt (wa pili kushoto), pamoja na Maofisa wake walioambatana naye kuwasilisha hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais akifanya mazungumzo na Balozi mpya wa Sweden hapa nchini na ujumbe wake, baada ya kuwasilisha hati zake za utambulisho.

  Mhe.Katarina Rangnitt, Balozi mpya wa Sweden hapa nchini akisikiliza wimbo wa taifa lake muda mfupi baada ya kuwasili ikulu jijini Dar es Salaam.
                                    ==================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.