Monday, September 7, 2015

Ujumbe kutoka China wakutana na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahaya, akizungumza na Naibu Mkuu wa Jimbo la Guangdong Nchini China, Mhe. Luo Jun wakati ujumbe kutoka Idara ya Mambo ya Nje ya Jimbo hilo, ulipomtembelea ofisini kwake leo  Septemba 7, 2015.
Naibu Mkuu wa Jimbo la Guangdong Nchini China, Mhe. Luo Jun akisisitiza jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahaya katika mazungumzo hayo.
Ujumbe kutoka Idara ya Mambo ya Nje ya Jimbo la Guangdong Nchini China wakifuatilia kwa makini mazungumzo hayo. Jimbo la Guangdong ndilo lenye miji mikubwa nchini China ya Guangzhou na Shenzhen na pia Jimbo hilo ndilo linaloongoza kuwa na idadi kubwa ya watu yapata milioni 106.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahaya,akizungumza jambo na Afisa Dawati - China, Medard Ngaiza wakati wa mazungumzo hayo.
 Mazungumzo yakiendelea
Naibu Katibu Mkuu akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.