Wednesday, January 11, 2023

TANZANIA YAAINISHA VIPAUMBELE VYAKE KWA MABALOZI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam hawapo pichani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam wanaonekana mbele katika picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (hayupo pichani) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na  waheshimiwa Mabalozi kutoka nchi za Ulaya na Amerika wanaoziwakilisha nchi  zao hapa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na wajumbe wa menejimenti wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na baadhi ya waheshimiwa Mabalozi na wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini



Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanisha vipaumbele vyake vya mwaka 2023 kwa Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao nchini.

Vipaombele hivyo vimeainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) alipokutana na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Januari, 2023.

“Misimamo ya Tanzania ni kuwa hatufungamani na upande wowote lakini pia Tanzania ni muumini wa uendelezaji wa ushirikiano wa kimataifa na kikanda. Tumeelezana vipaumbele vya Serikali hususani utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi na kuona ni jinsi gani mabalozi wanaweza kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi kwa manufaa ya pande zote,” alisema Dkt. Tax

Dkt. Tax aliongeza kuwa amesisitiza umuhimu wa maboresho yanayofanywa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ili kuboresha shughuli za kiuchumi, ambapo Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa na wameridhika na maboresho yanayofanywa na Serikali na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika sekta za kipaumbele zaidi ambazo Tanzania imeziainisha.

Kwa upande wake kiongozi wa Mabalozi nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed ameishukuru Serikali kwa kuainisha vipaumbele vyake kwa mwaka 2023 na kuahidi kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha kuwa inafika malengo yake iliyojiwekea kwa mwaka 2023.

“Kwa niaba ya Mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya Kimataifa, napenda kuahidi kuwa tutaendelea kushirikiana na wizara na Serikali kwa ujumla katika kuhakikisha inafikia viapombele na malengo yake iliyojiwekea kwa mwaka 2023,” alisema Balozi El Badaoui Mohamed

Mkutano huo ulilenga kufahamiana, kukumbushana na kutoa mwelekeo wa Serikali ya Tanzania katika masuala ya Diplomasia na mahusiano yake na nchi na taasisi mbalimbali kwa wana jumuiya hao wa kidiplomasia wanaowakilisha hapa nchini.

 

 

 

 

 

 

 




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.