Tuesday, January 24, 2023

DKT. TAX AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA APRM

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) amekutana na kuzungumza na watumishi wa taasisi ya Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Tax amewahakikishia ushirikiano watumishi wa APRM na kuwasihi kufanya kazi kwa bidii, kujituma na kutunza siri pamoja na kuweka maslahi ya taifa mbele.

“Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan haiko nyuma katika katika kusimamia masuala ya utawala bora, hivyo yote mliyonieleza hapa tutayafanyia kazi,” alisema Dkt. Tax

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Usimamizi la APRM, Prof. Hasa Mlawa ameishukuru Serikali kwa kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na APRM na kuahidi kuwa APRM itaendelea kufanya kazi kwa bidii nyakati zote kwa maslahi mapana ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kufanya kazi na taasisi yetu ya APRM, tunaahidi kutekeleza maelekezo yote kwa maslahi mapana ya taifa letu,” alisema Prof. Mlawa 

Awali Mtaalam Kiongozi wa APRM, Dkt. Rehema Twalib alisema kuwa tangu Tanzania ilipojiunga na APRM imetoa fursa kwa wananchi kuwasilisha maoni yao, kuweka wazi (transparency) taarifa za nchi pamoja na kusaidia kuimarishwa kwa huduma za kijamii.

Mtaalam Kiongozi wa APRM, Dkt. Rehema Twalib akiongea wakati wa kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) na wafanyakazi wa APRM katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Usimamizi la APRM, Prof. Hasa Mlawa akielezea jambo katika kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) na wafanyakazi wa APRM katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na watumishi wa taasisi ya Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na watumishi wa APRM kikiendelea katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.