Wednesday, September 11, 2019

BODI YA USHAURI YA UMOJA WA AFRIKA KUHUSU RUSHWA YAMTEMBELEA PROF. KABUDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na Bodi ya ushauri ya Umoja wa Afrika kuhusu rushwa ikiwa ni ziara ya Bodi hiyo kutathmini utekelezaji wa mkataba wa Umoja wa Afrika dhidi ya rushwa.
Ujumbe wa bodi hiyo umeongozwa na Bw. Miarom Begoto.
Tanzania ni mwenyeji wa Bodi hiyo kupitia mkataba wa uenyeji kati take na Umoja wa Afrika ambapo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ni mratibu mkuu na msimamizi wa uytekelezaji wa shughuli za bodi.

Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya ushauri ya Umoja wa Afrika kuhusu rushwa wakifuatilia mazungumzo kati ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagmba John Kabudi (Mb) (Hayupo pichani)

Sehemu ya Ujumbe wa wa Bodi ya ushauri ya Umoja wa Afrika kuhusu rushwa wakifuatilia mazungumzo kati ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagmba John Kabudi (Mb) (Hayupo pichani)

Kiongozi wa Ujumbe wa wa Bodi ya ushauri ya Umoja wa Afrika kuhusu rushwa Bw. Miarom Begoto akimkabidhi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagamba John Kabudi kijitabu chenye muongozo wa bodi hiyo.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagamba John Kabudi na kiongozi wa Ujumbe wa Bodi ya ushauri ya Umoja wa Afrika kuhusu rushwa wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi hiyo alioambatana nao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.