Tuesday, September 24, 2019

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA TAMASHA LA JAMAFEST LINALOENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akitoa mchango wake wakati wa warsha kuhusu namna utamaduni unavyochangia uchumi na maendeleo ya nchi za kanda ya Afrika Mashariki na namna ya kutangaza utalii kupitia sanaa na utamaduni iliyofanyika sambasamba na Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST linaloendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Tamasha hilo ambalo lilifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais tarehe 22 Septemba 2019 linatarajiwa kumalizika tarehe 28 Septemab 2019. 
Watoa mada na wachangiaji wakiwa kwenye warsha hiyo iliyojadili kwa kina masuala ya mila na tamaduni zinavyoweza kuchangia uchumi wa nchi za Afrika Mashariki
Sehemu ya washiriki wa warsha 
Washiriki wakifuatilia mada zilizowasilishwa kwenye warsha hiyo
Sehemu nyingine ya washiriki
Wanafunzi nao wakishriki warsha hiyo iliyojadili masuala kuhusu Utamaduni
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Dkt. Harrison Mwakyembe akipata maelezo kutoka kwa washiriki wa maonesho ya bidhaa zinazotengenezwa kwa mikono wakati wa tamasha la JAMAFEST linaloendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
Washiriki wa maonesho ya bidhaa mbalimbali za utamaduni wakiwa kwenye mabanda yao wakati wa Tamasha la JAMAFEST 2019
Sanaa za Utamaduni kama zinavyoonekana kwenye  Tamasha la JAMAFEST
Vinyago katika banda mojawapo la Tanzania
Sanaa za maonesho kama zinavyoonekana

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.