Saturday, September 7, 2019

MHE. RAIS MUSEVENI AHITIMISHA ZIARA YA SIKU TATU NCHINI

Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akizungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuhitimisha ziara yake ya siku tatu nchini kuanzia tarehe 5 hadi 7 Septemba 2019. Wakati wa ziara hiyo pamoja na mambo mengine, Mhe. Rais Museveni kwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli walifungua Kongamano la Kwanza la Biashara kati ya Tanzania tarehe 6  Septemba 2019.
Mhe. Rais Museveni na Mhe. Makamu wa Rais wakiendelea na mazungumzo yao huku Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia.
Waziri wa Elimu wa Uganda ambaye pia ni Mke wa Rais Museveni, Mhe. Janeth Museveni (kushoto) akiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Joyce Ndalichako wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Rais Museveni na Mhe. Makamu wa Rais
Mhe. Makamu wa Rais akiagana na Mhe. Rais Museveni huku Mama Janeth Museveni akishuhudia
Mhe. Makamu wa Rais akiagana na Mama Janeth Museveni
Mhe. Rais Museveni akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Kabudi
Mhe. Rais Museveni akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz Mlima
Mhe. Rais Museveni akifurahia burudani ya  kikundi cha  ngoma kilichkuwepo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ajili ya kumuaga Rais huyo
Mhe. Rais Museveni na Mhe. Makamu wa Rais wakiangalia moja ya kikundi cha ngoma wakati wa kumuaga Mhe. Rais Museveni
Mhe. Makamu wa Rais akiwaongoza viongozi wengine kupunga mkono wakati ndege iliyombeba Rais wa Uganda, Mhe. Museveni ikiondoka nchini kurejea Uganda
Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin akimsikiliza Balozi wa Uganda nchini, Mhe. Richard Kabonero mara baada ya kukamilisha hafla ya kumuaga Mhe. Rais Museveni kukamilika
Wadau mbalimbali waliojitokeza kumuaga Rais wa Uganda Mhe. Museveni. 
Wadau wengine
Wadau kutoka Jeshini nao walikuwepo uwanjani hapo
Wadau kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Sekta zingine wakifurahia kukamilisha kazi salama

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.