Sunday, September 22, 2019

MHE. MAKAMU WA RAIS AFUNGUA RASMI TAMASHA LA NNE LA SANAA NA UTAMADUNI LA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Uwanja wa Uhuru uliopo jijini Dar es Salaam leo tarehe 22 Septemba 2019 kwa ajili ya kufungua rasmi Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu kama JAMFEST 2019. Wengine katika picha ni pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza. Tamasha la mwaka huu limebeba kaulimbiu isemayo "Uanuai wa Kitamaduni: Msingi wa Utangamano wa Kikanda, Maendeleo ya Kiuchumi na Kukuza Utalii".

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mhe. Makamu wa Rais ametoa rai kwa wananchi wa Afrika Mashariki kuuenzi utamaduni wao ambao ni tunu kubwa kwa kuurithisha kwa vizazi vyao. Pia alitumia fursa hiyo kueleza kuwa, utamaduni ni nyenzo muhimu ya kuleta umoja, amani, ushirikiano na upendo miongoni mwa wana Jumuiya ya Afrika Mashariki. Pia sanaa na ubunifu ni sekta inayokua haraka na imetengeneza ajira kwa wingi kwa vijana na kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi za Jumuiya ya Mashariki  ikiwemo Tanzania. Mhe. Makamu wa Rais aliongeza kuwa, Tamasha la JAMAFEST tangu kuanzishwa kwake mwaka 2013 limekuwa ni chachu ya kuimarisha mtangamano. Zaidi ya washiriki 3000 kutoka Nchi Wnachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanashiriki Tamasha hilo.
Mhe. Makamu wa Rais akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akipiga ngoma kuashiria ufunguzi rasmi wa Tamasha hilo ambalo alitangaza kuwa linakwenda sambamba na Tamasha la Urithi la Tanzania. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mhe. Mwakyembe (kulia), Waziri wa Michezo wa Kenya, Mhe. Amina Mohammed (kushoto) na  Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Stephen Mlote (mwenye tai nyekundu kushoto)
Wananchi wa Dar es Salaam wakifuatilia matukio wakati wa ufunguzi rasmi wa Tamasha la Nne la JAMAFEST
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akizungumza wakati wa Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki huku wanachi wakimsikiliza
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya kutoka Tanzania, Bw. Peter Msechu akiwaobgoza wasanii wenzake kuimba wimbo maalum kuhusu JAMAFEST 2019
Mhe. Makamu wa Rais na Viongozi waliokuwa meza kuu wakiwa wamesimama kwa heshima wakati wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ukiimbwa wakati wa ufunguzi wa Tamasha la JAMAFEST 2019
Kikundi cha ngoma kutoka Tanzania kikitumbuiza
Kikundi cha ngoma kutoka Rwanda kikitumbuiza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Kikundi cha ngoma kutoka Burundi kikitumbuiza
Kikundi cha ngoma kutoka Kenya kikitumbuiza kwenye JAMAFEST 2019
Kikundi cha ngoma kutoka Uganda kikitumbuiza kwenye JAMAFEST 2019
Mhe. Makamu wa Rais akiagana na Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Bw. Nasib Abdul maarufu kama Diamond ambaye alitumbuiza kwenye Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Afrika Mashariki

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.