Saturday, September 28, 2019

TAMASHA LA JAMAFEST LAMALIZIKA KWA MAFANIKIO

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akitoa hotuba ya kufunga rasmi Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST ) lililofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 21 hadi 28 Septemba 2019. Tamasha hilo la aina yake lilizishirikisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo Burundi, Rwanda, Kenya, Uganda na Tanzania. Wakati wa Tamasha hilo vikundi mbalimbali vya sanaa na utamaduni kutoka nchi hizo vilishiriki. Katika hotuba yake Mhe. Balozi Iddi alitoa rai wadau wa sanaa na utamaduni kujikita kwenye ubunifu kwa ajili ya kukuza uchumi kupitia sanaa. Tamasha la JAMAFEST ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili limepangwa kufanyika mwaka 2021 nchini Burundi
Mhe. Balozi Iddi akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Christopher Bazivamo alipowasili kwenye Tamasha la JAMAFEST
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifuatilia hotuba ya Mhe. Balozi Iddi (hayupo pichani)

Sehemu ya wageni waalikwa wakiwemo viongozi wa dini wakiwa kwenye sherehe za ufungaji wa Tamasha la JAMAFEST
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa

Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akipata maelezo kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki kuhusu Banda la Maonesho la Wizara hiyo  alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho yaliyofanyika wakati wa Tamasha la JAMAFEST
Mhe. Balozi Iddi akipata maelezo kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii
Mhe. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimsikiliza mmoja wa washiriki wa maonesho alipotembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii
Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Zanzibar
Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye Banda la Rwanda

 

Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Burundi

Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Uganda

Msanii Mrisho Mpoto akitumbuiza wakati wa sherehe za kuhitimisha Tamasha la JAMAFEST
Wasanii kwenye JAMAFEST

Watoto kutoka Dodoma wakitumbuiza

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.