Monday, September 9, 2019

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CUBA ZIARANI TANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika mazungumzo na mgeni wake ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez. mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar Es Salaam.
Mazungumzo baina ya wawili hayo yamegusia mashirikiano katika nyanja za kidiplomasia,afya,elimu pamoja na viwanda.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimsikiliza mgeni wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez (hayupo pichani) Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar Es Salaam.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) (hayupo pichani) katika Mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki zilizopo jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez wakiwa katika mazungumzo kuhusu mashirikiano baina ya nchi hizo mbili. wengine pichani ni Wakurugenzi na maafisa kutoka Tanzania na Cuba wakifuatilia mazungumzo haya yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.