Friday, September 6, 2019

WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI AFUNGUA RASMI MKUTANO WA TATU WA TUME YA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA UGANDA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akitoa hotuba wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda  uliofanyika  kwa ngazi ya Mawaziri kwenye Ukumbi wa Mikutano katika Jengo la Mamlaka ya Bandari Tanzania jijini Dar es Salaam tarehe 5 Septemba 2019. Wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Mhe. Sam Kutesa (katikati),  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Uganda, Balozi Patrick Mugoya (kulia).
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Mhe. Sam Kutesa nae akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda.
Mhe. Prof. Kabudi akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tume ya pamoja ya ushirikiano
Sehemu ya Mawaziri wakifuatilia hotuba za Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania na Uganda (hawapo pichani)
Sehemu ya Mawaziri kutoka Uganda walioshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda
Makatibu Wakuu kutoka Wizara mbalimbali za Tanzania wakiwa kwenye mkutano wa tatu wa tume ya pamoja ya ushirikiano
Makatibu Wakuu kutoka Wizara mbalimbali za Uganda nao wakiwa kwneye mkutano wa tatu wa tume ya ushirikiano
Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz Mlima akiwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Wilbroad Kayombo kwenye Mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda 
Sehemu ya ujumbe wa Uganda ulioshiriki Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda


Sehemu ya ujumbe wa Tanzania nao ukiwa kwenye Mkutano wa Tatu wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza wakati wa mkutano uliofanyika kwa ngazi ya Makatibu Wakuu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Uganda, Balozi Patrick Mugoya nae akizungumza wakati wa mkutano uliofanyika kwa ngazi ya Makatibu Wakuu
Mkutano ukiendelea
Ujumbe wa Uganda

Ujumbe wa Tanzania


Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Caroline Chipeta (kulia) akijadiliana jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Bw. Wilbroad Kayombo pamoja na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Blandina Kasagama wakati wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda

Mhe. Prof. Kabudi akiagana na Mhe. Sam Kutesa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa tatu wa tume ya pamoja ya ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.