Tuesday, July 1, 2014

Mke wa Mfalme Mswati wa II wa Swaziland awasili nchini wa ziara

Ndege iliyombeba Mke wa kwanza wa Mfalme  Mswati ikiwasili katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Juliusa Nyerere jijini Dar es salaam.

Mke wa Kwanza wa Mfalme Mswati wa II wa Swaziland Malikia Nomsa La - Matsebula akiteremka katika ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mara baada ya kuwasili nchini kwa ziara.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akimpokea Malkia Nomsa La - Matsebula mara baada ya kuwasili nchini.
Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mtoto wa Mfalme Mswati II ambaye amefuatana na Malkia Nomsa kwenye ziara hapa nchini.
Malkia Nomsa La - Matsebula akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Raymond Mushi
Malkia Nomsa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji anayewakilisha pia nchini Swaziland, Mhe. Shamim Nyanduga
Afisa Mambo ya Nje Mwandamizi Bi. Hellen Kafumba akisalimiana na Malkia Nomsa
Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.