Wednesday, December 6, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Nigeria nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Nigeria nchini, Mhe. Dkt. Sahabu Isah Gada. Tukio hilo limefanyika Wizarani tarehe 06 Desemba, 2017.
Mhe. Dkt. Mahiga akionesha Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Gada mara baada ya kuzipokea.
Mhe. Dkt. Mahiga akiwa katika mazungumzo rasmi na Dkt. Gada
Sehemu ya ujumbe kutoka Ubalozi wa Nigeria.
Sehemu ya ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ukifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Mahiga na Balozi Gada (hawapo pichani). Kushoto ni Bw. Suleiman Saleh, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Bw. Nicholaus Joseph, Afisa Mambo ya Nje.
Mhe. Dkt. Mahiga akiagana na Balozi Mteule wa Nigeria nchini, Mhe. Dkt. Gada mara baada ya kumaliza mazungumzo yao
Mhe. Dkt. Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Balozi Gada na Mkewe mara baada ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi huyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.