Tuesday, December 19, 2017

Matukio yanayojiri katika ziara ya kikazi ya Balozi Mahiga nchini China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea jambo wakati alipokuwa katika mazungumzo rasmi na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming jijini Beijing.
Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming akisisitiza jambo alipokuwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt.Augustine Mahiga leo jijini Beijing.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa na ujumbe wake aliongozana nao katika ziara ya kikazi nchini China. Kutoka kushoto ni Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China, Kanali Remigius Ng'umbi anayefuata ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Thomas Kashililah na Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki.

Wajumbe wa pande mbili za China na Tanzania wakiwa katika mazungumzo.

Wajumbe wengine wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo. Kutoka kulia ni Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Malmeltha Mutagwaba, Naibu Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango kutoka Serikali ya Zanzibar, Bw. Khamis Omar 

Balozi Mahiga akitoa zawadi ya picha kwa Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming.

Mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango ya China
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipngo ya China, Bw. Ning Jizhe alipowasili ofisini kwake kwa ajili ya kufanya mazungumzo.

Ujumbe wa Tanzania na China wakijadiliana namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiano katika masuala ya uchumi, uwekezaji n biashara.

Bw. Jing Jizhe akionesha utayari wa nchi yake wa kushirikiana na Tanzania katika masuala ya maendeleo ya kiuchumi.
 Mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi
Balozi Mahiga na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Balozi Mahiga akiwa na katika mazungumzo na mmoja wa wawekezaji aliyedhmiria kuwekeza Tanzania.

Mwekezaji mwingine akisalimiana na Balozi Mahiga kabla ya kuanza kwa mazungumzo yao.

Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na aliyekuwa Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt, Lu Youqing

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.